Israel Mbonyi – Kaa Nami (Lyrics)
Ikiwa nimepata neema kwako, unikumbuke
Jicho lako liwe juu yangu nyakati zote
Wema wako unisindikize Hadi tamati
Hili ni ombi langu, nakumwagia moyo Ninachoomba kaa nami
ikiwa nimepata neema kwako
Kutakuwa milima haitaondolewa
Kutakuwa na mito na sitaweza kuvuka
Sio kila ombi litajibiwa nipendavyo
Sio kila wimbo utakaotuliza moyo
Nimekupata, nina mtetezi
Unionyeshe njia zako
Nikujue.
Ikiwa nimepata neema kwako, unikumbuke
Jicho lako liwe juu yangu nyakati zote
Wema wako unisindikize Hadi tamati
Hili ni ombi langu, nakumwagia moyo Ninachoomba kaa nami
ikiwa nimepata neema kwako
Kumbuka hayo mema niwaombeayo wanaonifurahia
maadui zangu nao, uwape kukujua
Uwabaliriki kwa utele uwanyeshee mvua
yamkini watapata kuona
Wapumue upendo.
Tunaoshiriki hii huduma,
uwape uamsho
Uwabaliriki kwa utele ,
Baba wala-hi-sishie.
Ikiwa nimepata neema kwako, unikumbuke
Jicho lako liwe juu yangu nyakati zote
Wema wako unisindikize Hadi tamati
Hili ni ombi langu, nakumwagia moyo Ninachoomba kaa nami
ikiwa nimepata neema kwako
Kwa maswali na majibu,
umasikini utajiri, usumbufu utulivu
Ewee Mwokozi kaa nami
Kwa kupanda kwa kushuka,
habari za kuvunja moyo
Kwa uzushi na uongo
Ewee Mwokozi kaa nami.
Ikiwa nimepata neema kwako, unikumbuke
Jicho lako liwe juu yangu nyakati zote
Wema wako unisindikize Hadi tamati
Hili ni ombi langu, nakumwagia moyo Ninachoomba kaa nami
ikiwa nimepata neema kwako
